Maisha ya nabii


(Katika hii ardhi tumekuumbeni na humo tutakurudisheni na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine??!!)



Yüklə 0,69 Mb.
səhifə15/15
tarix10.12.2017
ölçüsü0,69 Mb.
#34382
1   ...   7   8   9   10   11   12   13   14   15
(Katika hii ardhi tumekuumbeni na humo tutakurudisheni na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine??!!) (Taha - 55). Au hajui kuwa Allah kasema: (Je hatukuifanya ardhi kuwa ni yenye kukushanya (viumbe) * Vilivyohai na wafu) (Al-Mursalat 25-26). Je hajui kuwa kauli ya Allah isemayo : (Allah akamletea kunguru anayefukua ardhini ili amwonyeshe jinsi ya kuificha (kuizika) maiti ya nduguye) (Maida – 31); hajui yeye kuwa Aya hizi ni dalili ya mafundisho ya kuzikwa baada ya kufa? Je yeye hajui kuwa haya ni mafundisho aliyokuja nayo Mtume (s.a.w.)?!” Na unaweza kusema mengi kuliko haya ya kumfanya yeye kuwa hana analolijua na hali ya kuwa mambo hayakuwa hivyo, bali ni kule kufazaika kwake kwa kifo cha Baba yake Mpenzi, Rasulu Allah (s.a.w.). Na ndio maana baada ya Sayyidna Abu Bakr kuwasomea watu kauli ya Allah isemayo: (Na hakuwa Muhammad ila ni Mtume tu. Wamepita kabla yake Mitume (mingi) akifa au akiuawa ndio mtarudi nyuma kwa visigino vyenu (muwe makafiri) na atakayerudi nyuma kwa visigino vyake hatamdhuru Allah chochote. Na Allah atawalipa wanaoshukuru), kasema Ibnu Abbas kuwa:

وَاللهِ لَكَأنَّ النَاسَ لَمْ يَعْلَمُوْا أنَّ اللهَ أنْزَلَ هَذِهِ الآيَةَ حَتَّى تَلاَهَا أبُوْ بَكر

(Wallah kana kwamba watu walikuwa hawajui kuwa Allah kateremsha Aya hii ila baada ya kuisoma Abu Bakr).





1 - وَمَا مُحَمَّدٌ إِلاَّ رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِنْ قَبْلِهِ الرُّسُلُ أَفَإِيْن مَاتَ أَوْ قُتِلَ انْقَلَبْتُمْ عَلَى أَعْقَابِكُمْ وَمَنْ يَنْقَلِبْ عَلَى عَقِبَيْهِ فَلَنْ يَضُرَّ اللَّهَ شَيْئاً... (144)

2 - Ni wazi kuwa watu bado walikuwa na ukabila, kama ilivyo kawaida ya Warabu wengi. Kwa nini iwe Bani Hashim wote wamtake 'Ali, Bani Hashim mwanzao na wamkatae Abu Bakr?! Ukabila na utabaka ndio yalilokuwa matatazo sugu kwa Waislamu hadi kupelekea kuundika madhehebu tafauti. Na tatizo hili bado linaendelea hadi leo: watu hawatazami Allah anasema nini wala nani anastahiki kuwa kiongozi, bali wanatazama watu wa makabila yao wanasema nini, kisha wanawatetea kwa hali yoyote wakiwa ni madhalimu au wakiwa ni wenye kudhulumiwa. Wa Allahu Al-Musta'an!

1 - Katika jambo hili la Ukhalifa kila mmoja alijiona kuwa yeye anastahiki zaidi kuliko mwengine. Muhajirina walijiona kuwa wao wanastahiki kuliko Ansari na Ansari vivyo hivyo. Na katika haya kuna dalili tosha kuwa Mtume (s.a.w.) hakuusia kuwa ukhalifa baada yake uwe wa Sayyidna Ali wala wa mwengine, ingawa aliashiria – kwa mujibu wa riwaya sahihi ya Bukhari – kuwa Abu Bakr ndiye atayeshika ukhalifa na baada yake ni 'Umar, lakini hio haikuwa amri. Na kwa sababu hii, ndio maana utaona kuwa kila mmoja alikuwa na watu waliompendelea kuwa Khalifa pasina kutoa andiko lolote kutoka kwa Mtume (s.a.w.) kuwa fulani ndiye aliyechaguliwa na Mtume (s.a.w.) kuwa Khalifa baada yake, bali hoja zote zilikuwa kwa misingi ya ukabila na ukaraba (ujamaa na Mtume s.a.w.) na kufadhilishana baina yao. Na ndiyo maana utaona katika kuchaguliwa Sayyidna Uthman kuwa Khalifa alisema Miqdad kuwa: "أتُبَايِعُوْنَ رَجُلاً لَمْ يَشْهَدْ بَدْرًا؟!" “Hivyo munamchagua mtu ambaye hakuhudhuria (vita vya ) Badr?!” Kwa hivyo, yeye aliona kuwa Sayyidna Uthman hafai kwa sababu hakuhudhuria vita vya Badr: si kwa sababu hakuusiwa. Na haya aliyasema katika kumpigia kampeni rafiki yake kipenzi Sayyidna Ali. Na kilichosahihi ni kuwa Sayyidna Ali mwenyewe juu ya kuwa alijiona kuwa kadhulumiwa – kama inavyodaiwa – lakini hakutoa hoja ya kuwa yeye kausiwa kuwa Khalifa baada ya Mtume (s.a.w.). Bali tunakuta riwaya inayosimuliwa na Wanavyuoni wa Kishia kwamba Sayyidna Ali na Abbas waliingia kwa Mtume (s.a.w.) wakati alipozidiwa wakamwambia: “Ewe Mjumbe wa Allah tuchagulie Khalifa akasema: “La mimi nahofia mukaja mukafarikiana kama walivyofarikiana Bani Israili kutokana na Harun, lakini Allah akijua kwamba nyoyoni kwenu kuna kheri basi atakuchagulieni” Sh. Ahmad Al Katib Tawatur Al Fikri Al Siyasy Al Shi’i uk. 19. Naye kanukuu Riwaya hii kutoka katika kitabu “Al- Shafi” cha Sharif Al Murtadha. Na lililowazi zaidi ya hilo na ambalo limekubaliwa na Uma mzima ni ile Sulhu baina ya Al-Imamu Al-Hasan bin Ali na Muawiya kwa sharti kwamba MU'AWIYA AKIFA UKHALIFA UWE KWA NJIA YA SHURA. Haya yote yanaonesha wazi kuwa Ahlu Al-Bayt wenyewe walikuwa wakiizingatia Shura kuwa ndio njia pekee ya kuteuliwa Khalifa wa Kiislamu, vyenginevyo Imam Hasan asingelisisitiza hivyo. Kwa hivyo, ni wazi kuwa Mtume (s.a.w.) hakuchagua Khalifa baada yake. Na utakapotizama msimamo waliokuwa nao Muhajirina na Ansar unazidi kuthibitisha hayo, kwani kukutana kwao na kumchagua Khalifa wa Uislamu kunapingana na kauli ya kuwa Mtume (s.a.w.) kausia. Na kwa hivyo, Ali mwenyewe kanena havi: “Kilichowajibu katika hukumu ya Allah na hukumu ya Uislamu kwa Waislamu, baada ya kufa Imamu wao au kuuliwa… wasifanye kitu wala wasizuwe jambo wala wasitangulize mkono wala mguu wala wasianze chochote kabla hawajajichagulia Imamu mwenye kujizuia (na machafu) mjuzi, mnyenyekevu mwenye maarifa ya hukumu na Suna” . Almajlisi Biharu Al Anwaar j. 8 uk. 555 chapa ya zamani.

2 - Walinganiaji wengi waliowapinzani wa Abu Bakr na 'Umar wanaipotoa mafuhumu sahihi ya sehemu hii kwa kusema: ‘Baada ya kufa Mtume (s.a.w.) tu wakakutana mabwana wakubwa huko kwenye Saqifa kwenda kugombania ukubwa na huku wakauwacha Mwili Mtukufu wa Bwana Mtume (s.a.w.) pasina kuujali, na hakuna aliyeshughulika naye isipokuwa Imam Ali na Abbas na Al Fadhil bin Abbas’. Yaani wanataka kuonesha kuwa hao waliokutana kwa ajili ya kumchagua Khalifa ni watu wenye uchu wa madaraka na vyeo, na walengwa hasa hapa ni Sayyidna Umar na Sayyidna Abu Bakr, kwani falsafa za aina hii zenye ushawishi katika ulinganiaji hutumika zaidi linapotokea jambo lenye kuwahusu wao. Lakini utakapotizima mafundisho ya Uislamu utaona kuwa walivyofanya Masahaba ndivyo hasa ilivyokuwa ikitakikana, kwani:

1) Wanaostahiki kuishughulikia maiti ni watu wa familia: si watu wa nje na hivyo ndivyo ilivyokuwa – Ali na Abbas na Al Fadhil bin Abbas ndio watu wa karibu zaidi kwa Mtume (s.a.w.) kidamu, kwa hivyo wao ndio wenye haki ya kumkosha.



2) Uislamu umefundisha kwamba atakapokufa tu kiongozi wao basi wakutane Waislamu na kumchagua mwengine pasina kuchelewa kama Sayyidna Ali alivyosema: “Kilichowajibu katika hukumu ya Allah na hukumu ya Uislamu kwa Waislamu, baada ya kufa Imamu wao au kuuliwa… wasifanye kitu wala wasizuwe jambo wala wasitangulize mkono wala mguu wala wasianze chochote kabla hawajajichagulia Imamu…”. Na hii ni riwaya ya Kishia. Sasa sijui ni kosa gani walilolifanya wale waliokimbilia katika Saqifa ikiwa hivi ndivyo inavyotakiwa.





Yüklə 0,69 Mb.

Dostları ilə paylaş:
1   ...   7   8   9   10   11   12   13   14   15




Verilənlər bazası müəlliflik hüququ ilə müdafiə olunur ©muhaz.org 2024
rəhbərliyinə müraciət

gir | qeydiyyatdan keç
    Ana səhifə


yükləyin